Menu
in , , , ,

Man U ushindi kidogo, muhimu!

 
Manchester United wamepata ushindi mwembamba wa 1-0 dhidi ya Real Sociedad.
Wakicheza nyumbani katika Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa Jumatano, Man U walifanya kazi ya ziada kuepuka sare au kichapo, na hata bao lao walisaidiwa na mchezaji wa Sociedad, Inigo Martinez aliyejifunga katika dakika ya pili tu ya mchezo.

Walau ushindi huo ni faraja kwa kocha David Moyes ambaye ana wakati mgumu katika Ligi Kuu ya England, na Jumamosi iliyopita aliambulia sare ya 1-1 dhidi ya Southampton katika dimba la Old Trafford.

Mechi hiyo imekuja muda mfupi baada ya kocha aliyeng’atuka Manchester, Alex Ferguson kuzindua kitabu cha wasifu wake na masuala ya soka.

Sociedad waligangamala mbele ya washabiki wao 6,000 waliosafiri kutoka kwao wanakocheza Ligi Kuu ya Hispania – La Liga. United walishika roho zao pale mkwaju wa Antoine Griezmann ulipogonga mwamba, nusura asawazishe bao.

Katika mechi nyingine za ligi hiyo ya mabingwa,  RSC Anderlecht waliangukia pua mbele ya Paris Saint Germain walipochabangwa 5-0, CSKA Moscow wakalala 2-1 nyumbani walipowakaribisha Manchester City na Bayern Leverkusen wakawakandamiza Shaktar Donetsk  4-0.

Galatasaray ya Roberto Mancini walipata ushindi wa 3-1 dhidi ya FC Copenhagen, Real Madrid wakawafunga Juventus 2-1, Benfica wakaenda sare ya 1-1 na Olympiakos wakati Bayern Munich wakiwagaragaza Viktoria Plzen 5-0.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version