Menu
in , ,

Man City, Spurs zasonga mbele

 
Manchester City na Tottenham Hotspur zililazimika kufanya kazi ya zaida usiku wa Jumatano kufuzu robo fainali ya Kombe la Ligi.

Wakati Manchester City walibanwa na Newcastle hadi muda wa ziada, Spurs walipelekeshwa hadi hatua ya penati na Hull.

Newcastle walielekea kupoteza stamina katika muda wa ziada, ambapo walikubali mabao ya Edin Dzeko dakika ya 99 na Alvaro Degredo dakika ya 105 baada ya kuwa suluhu katika dakika 90 za kawaida.

Ulikuwa mchezo mkali na wa kuvutia, ambapo Newcastle walionesha kudhamiria kusonga mbele kwa kutengeneza nafasi nyingi za kufunga, na mojawapo Shola Ameobi alimlazimisha kipa namba mbili wa City, Costel Pantilimon kufanya kazi ya ziada.

Kocha wa Manchester City, Manuel Pellegrini alisema timu yake ilistahili ushindi, ikiwa ni siku chache baada ya kukubali kichapo kutoka Chelsea kwenye Ligi Kuu ya England (EPL).

Katika mechi nyingine, Spurs walitumia mikwaju ya penati kuwafurusha Hull, baada ya kwenda sare ya mabao 2-2 katika dakika 120.

Kwenye penati, Spurs walifunga nane na Hull saba.

Robo fainali itazikutanisha timu za Leicester dhidi ya Manchester City; Stoke na Manchester United wakati ama Sunderland au Southampton ndio watacheza na Chelsea huku Spurs wakipangwa na West Ham.

Mechi hizo zitachezwa katika wiki inayoanza Desemba 16 mwaka huu.
 

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version