in

Kombe la Mpira wa Kikapu kufanyika Oktoba Dar

MASHINDANO ya mpira wa kikapu ya Kombe la Taifa yatafanyika jijini Dar es Salaam kuanzia Oktoba 19 hadi 25, kwa mujibu wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu Tanzania, TBF.

Katibu Mkuu wa TBF, Lawrence Cheyo alisema mashindano hayo yatafanyika baada ya mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.

“Tumeona tufanye mashindano haya baada ya mwezi mtukufu wa ramadhani ili tuyafanye kwa uhuru zaidi na wachezaji wakiwa na nguvu,” alisema

Alisema mashindano hayo yatashirikisha mikoa yote ya Tanzania Bara.

”Mikoa ianze kujiandaa mapema kuanzia nauli ya kuja katika mashindano na ya kurudi, pia kila timu iwe na wachezaji wasiozidi 12, tunatarajia mikoa husika itazisaidia timu fedha kwa ajili ya mashindano.”

”Tunataka mashindano ya mwaka huu yawe na msisimko hivyo timu zijitahidi kufanya mazoezi ya nguvu kuhakikisha zinafanya vizuri,” alisema

Alisema mwisho wa mikoa kuthibitisha ushiriki wao ni Agosti 30 na iwapo timu haitathibitisha ifikapo wakati ule itaondolewa mashindanoni. Bingwa mtetezi wa michuano hiyo ni Mkoa wa Dar es Salaam kwa wanaume na wanawake.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Ziara ya Real Madrid Tanzania yaibuka upya Bungeni

Premier League – Villa: Barry transfer saga over