in , , ,

Kimetto rekodi mpya Marathon

Raia wa Kenya, Dennis Kimetto amevunja rekodi ya mbio za Marthon jijini Berlin, Ujerumani.

Kimetto (29) ameibuka mshindi kwa kukimbia kwa muda wa saa mbili, dakika mbili na sekunde 57, akivunja rekodi ya awali iliyokuwa ikishikiliwa na Mkenya mwenzake, Wilson Kipsang, aliyetumia muda wa 2:03:23 mwaka mmoja uliopita.

Mpinzani wake kwenye mbio hizo za Berlin, naye Mkenya, Emmanuel Mutai alikimbia kwa 2:03:13.

Kimetto alisema kwamba anajihisi furaha na fahari kubwa kwa kushinda mashindano hayo yaliyokuwa magumu na kwamba alikuwa vizuri tangu mwanzo, akidhamiria kuvunja rekodi ya dunia.

Kimetto amesema kadiri miaka inavyokwenda rekodi zinazidi kuvunjwa, akasema labda wakati ujao atatumia saa mbili na dakika moja tu.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Man United wapumua, Rooney out

TP Mazembe nje Afrika