Menu
in

Kiingilio cha kuwaona stars Mwanza ni mzigo kwa wananchi!

KIINGILIO cha mechi ya timu ya Tanzania,Taifa Stars na Uganda, The Cranes, itakayochezwa leo kwenye Uwanja wa CCM Kirumba kimelalamikiwa na mashabiki wa soka hapa kuwa ni kikubwa.

Shirikisho la soka Tanzania, TFF limetangaza kuwa watakaotaka kuuona mchezo huo watalazimika kulipa sh,5,000 kwa mzunguko na sh,20,000 kwa jukwaa kuu.

Nizar Khalfan

Baadhi ya mashabiki wameanza kugwaya na kupanga kuusikiliza mchezo huo kupitia redio na kwa kile walichodai kuwa kiingilio ni kikubwa.

Taarifa mbalimbali zilizokuwa zikipatikana jijini humo kutoka kwa mashabiki na wapenzi wa soka tangu kutangazwa kwa kiingilio hicho zilikuwa zinasema kwamba kiingilio hicho ni kikubwa mno kiasi kwamba mashabiki wengi hawataweza kumudu hali ambayo inaweza kupunguza mapato kwa timu hizo.

Msemaji wa TFF nchini Florian Kaijage aliviomba vyombo vya habari jana jijini hapa kuwaelimisha wapenzi wa soka kuwa hicho ni kiingilio cha kawaida kutokana na gharamaza uendeshaji wa mechi hiyo.

Kaijage alisema kuwa kiingilio hicho sio mara ya kwanza kutumika kwa mechi kubwa katika jiji la Mwanza ispokuwa vyombo vya habari vinatakiwa kusidia TFF kuwaelimisha wapenzi ili wajitokeze kwa wingi.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version