in , ,

Kenya mabingwa wapya Chalenji

Wenyeji Kenya wamefanikiwa kunyakua ubingwa wa Chalenji kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati.

Harambee Stars walisherehekea vyema miaka 50 ya uhuru wa Kenya kwa kuwafunga Sudan 2-0 kwenye mechi kali iliyochelewa kuanza kutokana na mvua na uwanja wa Nyayo kujaa maji.

Nahodha wa Kenya, Allan Wanga ndiye alifunga mabao yote mawili na kuwapa ubingwa baada ya kuukosa tangu 2002.

Hili ni kombe la kwanza pia kwa Kocha Adel Amrouche tangu alipokabidhiwa timu hiyo Februari mwaka huu.
Wanga ni mchezaji wa AFC Leopards ambayo pamoja na Gor Mahia zimerejea kwenye kilele cha mafanikio ya soka baada ya kutupwa nje kwa miaka mingi.

Timu ya taifa ya Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars walishindwa kupata nafasi ya tatu baada ya kufungwa na Zambia kwa mikwaju ya penati.
Stars walitangulia kufungwa bao ndani ya muda wa kawaida kabla ya kusawazisha lakini zilipokuja changamoto za penati Chipolopolo wakawapopoa kwa penati 6-5. Kipa wao aliokoa penati tatu.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Chelsea washika usukani

Van Persie nje mwezi mzima