Menu
in

Hasheem Thabeet atua Blazers

NYOTA pekee wa Tanzania anayecheza mpira wa kikapu katika ligi ngumu, yenye mvuto na utajiri mkubwa kwa ngazi za klabu duniani, Ligi ya Kikapu ya Marekani (NBA), Hasheem Thabeet amenyakuliwa na klabu ya Portland Trail Blazers inayoshiriki katika ligi hiyo.

Sasa akiwa na umri wa miaka 25, Thabeet ambaye hadi anatimiza umri wa miaka 15 alikuwa hajawahi kucheza mpira wa kikapu, ametua Blazers akitokea Houston Rockets akibadilishwa na mchezaji mwingine Marcus Camby.

Uhamisho huo ulikamilika jana ambayo ilikuwa siku ya mwisho iliyowekwa na NBA kwa ajili ya klabu zinazocheza ligi hiyo kufanya utaratibu huo wa kubadilishana wachezaji.
Mlinzi Jonny Flynn, pia amejiunga na klabu ya Portland Trail Blazers kama sehemu ya utaratibu huo, Thabeet ambaye sasa amechukuliwa na Blazers kabla alichukuliwa na Houston Februari mwaka jana, akitokea Memphis na alifanikiwa kuichezea Rockets mechi tano pekee katika msimu huu wa ligi.
“Tunatazamia kuwa yale yatakayofanywa na Jonny pamoja na Thabeet yanaweza kuleta mafanikio katika timu yetu na pia tunamshukuru Marcus kwa mchango alioutoa kwa kipindi cha misimu mitatu aliyokuwa nasi na tunamtakia kila la heri huko alikoenda,” alisema Kaimu Meneja Mkuu wa Blazers, Chad Buchanan.
Katika michezo 120 ya misimu mitatu akiwa na klabu za Memphis na Houston, Thabeet anayetajwa mmoja wa wachezaji tajiri ukanda wa Afrika Mashariki, amekuwa na wastani wa kufunga pointi 2.2.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version