in

Hamis Kitambi anahitaji msaada wetu…

Hamisi Kitambi ni mmoja wa wanamuziki wakongwe na hazinakubwa iliobakia hapa nchini Tanzania ,bwana Hamisi Kitambi mtunzi wa nyimbo nyingi , mojawapo ya nyimbo zake ni ule wimbo mzuri maarufu kwa jina ” Mpenzi wangu mwenye rangi ya Chungwa” kwa wale wenye kumbukumbu wanajua radha ya utamu wa wimbo huo.

kitambis

Mkongwe huyu Hamisi Kitambi amefanya kazi na bendi nyingi zikiwamo Tabora jazz,Unyanyembe band,  KIKO KIDS, Dar-es-salam JazzBand, Western Jazz. Hadi anapata ajali ya gari alikuwa Juwata (OTTU) Jazz sasa Msondo Ngoma aka Baba ya Muziki. Mwanamziki huyu mkongwe Hamisi Kitambi alipata ajali akiwa katika gari yeye na wanamziki wenzie wa  Msondo Ngoma, walipokuwa safarini Tanga!.Mzee Hamisi Kitambi kama anavyoonekana pichani,miguu yote imevunjika na amewekewa vyuma,cha kusikitisha zaidi ni kuwa, tangu apate ajali ndio katupwa tii! ,Huduma muhimu hana, mtaji wa masikini ni MIGUU YAKE nayo ndio kama anavyoonekana.

kitambiddd

Tujaribu kumsaidia mzee wetu huyu mwanamuziki mkongwe Hamisi Kitambi anapatikana  kwa simu hii Dar 0713576475.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Pompey players given wages pledge

Mijibwa na Bar za Ulaya!!