Menu
in , , , ,

Chelsea wamtwaa Mohamed Salah

Klabu ya Chelsea imemsajili winga wa Basel ya Uswisi kutoka Misri, Mohamed Salah aliyewatesa kwenye mechi za Ligi ya Europa.

Usajili huo unadaiwa kuwa na gharama ya kadiri ya pauni milioni 11 na unakuja wakati klabu hiyo imemwachia kiungo mchezeshaji Juan Mata kwenda Manchester United kwa pauni milioni 37 hivi ambazo si kawaida Man U kuziachia kihivyo.

Salah (21) alitarajiwa kuchukuliwa vipimo kiafya hapo Stamford Bridge na pia kukutana naye kwa ajili ya makubaliano baina yao na yeye kwa mafao yake.

Hatua hii inakuja wakati Liverpool walishaanza mazungumzo na Basel kwa ajili ya kumchukua raia huyo wa Misri kwa ajili ya kumsajili kwenye dirisha dogo Januari hii.

Chelsea tayari wamemsajili Nemanja Matic. Salah aliwafunga Chelsea kwenye nusu fainali ya Europa mwaka jana kabla ya kupata bao pekee dhidi ya klabu hiyo ya kocha Jose Mourinho Desemba katika Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version