Menu
in , ,

Bayern Munich mabingwa Ujerumani


*Watawazwa mechi sita kabla ligi kumalizika

Bayern Munich wametawazwa mabingwa wa Ujerumani, wakiwa wamesaliwa na mechi sita mkononi.
Bayern wameweka rekodi hiyo ya aina yake na kuwavua ubingwa Borussia Dortmund Jumamosi hii, kwa kuwachapa Eintracht Frankfurt bao 1-0.
Hii ndiyo rekodi ya kwanza kwa timu katika Ligi Kuu ya Ujerumani – Bundesliga kutwaa ubingwa mapema kiasi hiki.
Huu ni ubingwa wa 23 kwa Bayern, ambao pia wanaendelea vyema kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, wakienda Italia kurudiana na Juventus Jumanne, wakiwa mbele kwa mabao 2-0 waliyopata nyumbani wiki iliyopita.
Aliyevuta ubingwa mapema Bayern ni nyota wao, Bastian Schweinsteiger, aliyefunga bao pekee Jumamosi, ukiwa ni ushindi wa 24 kati ya mechi 28 msimu huu.
Bayern hawakupata kutwaa kombe kubwa tangu 2010, na hii ni zawadi kubwa kwa kocha Jupp Heynckes anayeng’atuka, na nafasi yake itachukuliwa na aliyekuwa kocha wa Barcelona, Joseph ‘Pep’ Guardiola.
“Hii ni timu kubwa yenye kocha wa aina yake, ni furaha kubwa kutwaa taji hili,” akasema Schweinsteiger.
Ubingwa huo umekuja licha ya Heynckes kupumzisha baadhi ya nyota wake kwa ajili ya mechi hiyo ya marudiano dhidi ya Wataliano.
“Si jambo la kawaida kutwaa kombe hili baada ya mechi 28 tu, ni furaha isiyo kifani. Moja ya tunu tulizoonyesha msimu huu ni kwamba hii ni timu kubwa.
“Ukubwa huu unatokana na wadau wake kuwa wana uelewano mkubwa, hivyo kwamba tuna uhakika wa kutwaa chochote katika Ligi ya Mabingwa” akasema kocha Heynckes.
Ushindi wa jana wa Borussia Dortmund – mabingwa wa misimu miwili iliyopita haukuweza kuwasaidia kurejesha ndoto za kutetea taji. Waliwafunga Augsburg mabao 4-2.
Kiungo wa Dortmund aliyetoka Liverpool Januari, Nuri Sahin, alisema hawana hiana na ubingwa kwenda Bayern na wanawapongeza kwa mafanikio yao.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version