Menu
in , , ,

Arsenal wapaa

Arsenal wapaa

 

Arsenal wamepata ushindi wao wa nane mfululizo katika Ligi Kuu ya England (EPL) na kushikilia nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi.

 

Washika Bunduki wa London wakicheza ugenni kwa Burnley walifanikiwa kushinda 1-0 kwa bao la kiungo wao, Aaron Ramsey.

 

Burnley wana wakati mgumu kwa sababu wanabaki nafasi ya pili kutoka mkiani huku Arsenal wakiwa nafasi ya pili kwa pointi 66 dhidi ya 70 za Chelsea wanaongoza licha ya vijana wa Jose Mourinho kuwa na mechi mbili mkononi.

 

Katika mechi nyingine Totenham Hotspur wakicheza nyumbani walipotezewa na Aston Villa kwa kufunga 1-0, ambapo kocha wa Villa ndiye aliyefukuzwa kazi Spurs kwa madai hana ufanisi.

 

Swansea walikwenda sare ya 1-1 na Everton, Southampton wakawazidi Hull nguvu kwa 2-0, Sunderland wakapata zahama ya kupigwa 4-1 na Crystal Palace, West Bromwich Albion wakapoteza kwa Licester kwa 3-2, huku West Ham wakitoshana nguvu 1-1 na Stoke.

 

Leo mtoto hatumwi dukani, kwa sababu Manchester United wanawaalika watani wao wa jadi jijini hapo, Manchester City katika mechi ya kukata na shoka huku Chelsea wakicheza na timu dhaifu ya QPR.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version