in

Angetile kuanza kazi TFF leo

Rais wa TFF, Leodegar Tenga

Katibu mkuu mpya wa TFF, Angetile Osiah, anatarajiwa kuripoti leo katika ofisi za shirikisho hilo la soka Tanzania kwa ajili ya kuanza kibarua chake kipya alichokiomba hivi karibuni.

Osiah aliteuliwa na Kamati ya Utendaji ya TFF kushika nafasi hiyo iliyoachwa wazi na Fredrick Mwakalebela, baada ya kuonekana kuwa na uwezo zaidi ya waombaji wengine wanne waliofika hatua ya fainali ya mchujo.

Hata hivyo, TFF kupitia kwa Rais wake, Leodegar Tenga haikuwa tayari kuwataja waombaji wengine waliojitokeza na kufika hatua hiyo ya tano bora.

Akizungumza na gazeti hili, Osiah alisema kuwa kabla ya kuanza kazi anatarajia kukutana na watendaji wengine wa shirikisho hilo kwa ajili ya kufahamiana na baada ya hapo atakutana na waandishi wa habari kwa ajili ya kueleza mikakati yake.

Osiah alisema kuwa mara baada ya kuripoti atasaini mkataba wa ajira wa miaka miwili na ana anaamini atakapopata ushirikiano kutoka kwa wadau mbalimbali wa soka hapa nchini, malengo yaliyopo yatafikiwa.

Siku chache baada ya kutangazwa kuwa katibu mkuu mpya, gazeti hili lilifanya mahojiano na Osiah ambapo alisema kuwa msingi wa kazi zake utakuwa ni kutekeleza kanuni, sheria na maagizo ya mkutano mkuu ambao ndio unaotoa dira na muelekeo sahihi.

Osiah alisema pia atahakikisha katika uongozi wake hapendelei klabu yoyote na zote atazipa haki sawa kama katiba na kanuni husika za mashindano zinavyoeleza.

Aliongeza kuwa katika uongozi wake atafanya kazi bila ya kuyumbishwa na atakuwa na msimamo, jambo analoamini litasaidia kuinua soka la nchini kuanzia klabu hadi taifa.

Mbali na Osiah, Boniface Wambura aliyekuwa Mhariri Mtendaji wa gazeti la Jambo Leo, naye anatarajiwa kuanza kibarua chake cha Afisa Habari wa shirikisho hilo pamoja na Jimmy Kabwe ambaye ni Mkurugenzi wa Kwanza wa Masoko na Matukio.

Enhanced by Zemanta

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Let us make 2011 a successful year

Premier League – Duo off as Man City hold Arsenal