Menu
in

4,000 wachuana Kilimanjaro Marathoni

Tanzaniasports::Where Sports People Meet


 

Zaidi ya wanariadha 4,000 wanatarajia kutoana jasho katika mashindano ya Kilimanjaro Marathoni yatakayofanyika leo mjini hapa.

Kwa mujibu wa waandaaji Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo George Mkuchika ndiye anayetarajia kuwa mgeni rasmi katika mbio zitakazoshirikisha wanariadha kutoka ndani na nje ya nchi, akiwemo mshindi wa mwaka jana Andrew Cyliv aliyetumia saa 2:18.47.

Hata hivyo, muda wa wastani wa kumaliza mbio za kimataifa za marathon zenye hadhi zaidi ni saa 2:08.

Kwa mujibu wa daftari la usajili, mshindi wa tatu wa mbio za nyika za Afrika Mashariki zilizofanyika mjini hapa wiki iliyopita Jumanne Tulway naye amejiandikisha kwa mashindano hayo.

Mbali na mbio za marathon, pia kutakuwa na mbio za nusu marathon ambazo miongoni mwa watakaoshiriki ni Martine Sulle.

 

Mshindi wa kwanza katika mbio za kilometa 42 (marathoni) atazawadiwa shilingi milioni 3 kwa wanawake na wanaume.

Mashindano hayo yatashirikisha wanariadha kutoka Tanzania, Kenya, Uganda, Zambia, Canada, Marekani, Afrika Kusini na Rwanda.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version