in

4,000 wachuana Kilimanjaro Marathoni

Tanzaniasports::Where Sports People Meet


 

Zaidi ya wanariadha 4,000 wanatarajia kutoana jasho katika mashindano ya Kilimanjaro Marathoni yatakayofanyika leo mjini hapa.

08-hk.jpg

Kwa mujibu wa waandaaji Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo George Mkuchika ndiye anayetarajia kuwa mgeni rasmi katika mbio zitakazoshirikisha wanariadha kutoka ndani na nje ya nchi, akiwemo mshindi wa mwaka jana Andrew Cyliv aliyetumia saa 2:18.47.

Hata hivyo, muda wa wastani wa kumaliza mbio za kimataifa za marathon zenye hadhi zaidi ni saa 2:08.

Kwa mujibu wa daftari la usajili, mshindi wa tatu wa mbio za nyika za Afrika Mashariki zilizofanyika mjini hapa wiki iliyopita Jumanne Tulway naye amejiandikisha kwa mashindano hayo.

Mbali na mbio za marathon, pia kutakuwa na mbio za nusu marathon ambazo miongoni mwa watakaoshiriki ni Martine Sulle.

 

Mshindi wa kwanza katika mbio za kilometa 42 (marathoni) atazawadiwa shilingi milioni 3 kwa wanawake na wanaume.

Mashindano hayo yatashirikisha wanariadha kutoka Tanzania, Kenya, Uganda, Zambia, Canada, Marekani, Afrika Kusini na Rwanda.

Report

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Premier League – What the managers said

Will Tanzania boxers qualify for Olympic Games?