Menu
in

Walimu kufufua michezo iliyokufa

Tanzaniasports::Where Sports People Meet


By Idda Mushi, PST, Morogoro

Michezo mingi ambayo imekufa ama kusahaulika ni rahisi kufufuliwa upya kupitia mpango wa mafunzo ya michezo kwa walimu mashuleni ambao wataweza kumudu kufundisha wanafunzi na hatimaye kusambaa katika maeneo mbalimbali nchini.

Baadhi ya walimu wa shule za msingi na Sekondari walisema hayo wakati wakiongea na PST mjini hapa wakati wa mafunzo ya mchezo wa kuruka upondo ikiwa ni sehemu ya mafunzo ya riadha yanayotolewa na mtaalamu kutoka nchini Ujerumani.

Walimu hao walisema kuwa mchezo kama upondo uliokuwa umekufa itakuwa ni rahisi kujulikana na kuanza kuchezwa upya baada ya wao kupata elimu ambayo wanakusudia kuitoa kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari na baadaye uweze kuenea katika sehemu mbalimbali nchini.

Naye mkufunzi wa maswala ya michezo kutoka Ujerumani, Peter Thumm alisema kuwa Tanzania ni nchi yenye vipaji vingi, ambapo kama vikitumiwa vyema nchi inaweza kupata medali nyingi katika fani ya michezo ya aina mbalimbali.

Alisisitiza kuwa iwapo vijana watafundishwa michezo mbadala wanaweza kuwa miongoni mwa wanamichezo wazuri watakaoweza kuiletea sifa nchi kwa kukusanya medali nyingi kwenye michezo hiyo hususani katika michuano ya Jumuiya ya Madola na michuano mingine.

Mafunzo hayo yameshirikisha walimu 10 kutoka mkoa wa Morogoro na yanahusisha walimu waliofaulu kwenye kozi ya kwanza iliyohusu maswala ya riadha ambayo ilimalizika hivi karibuni.

Mafunzo hayo yanalenga walimu hao kujenga uwezo wa kufundisha wanafunzi mashuleni juu ya maswala ya michezo ya aina mbalimbali ambayo kama wakimudu vyema inaweza kuitangaza nchi kitaifa na kimataifa.

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

Leave a Reply

Exit mobile version