in , ,

Ujerumani wawapopoa Poland

Euro 2017

Ujerumani wamekwea kwenye uongozi wa Kundi D kwenye mechi za kufuzu kwa fainali za Euro 2016, baada ya kuwafunga Poland 3-1.

Yalikuwa mabao ya Thomas Muller aliyefunga kirahisi kwa mpira wa juu huku shujaa wao aliyewapa bao kwenye fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil mwaka jana, Mario Gotze akifunga mawili.

Poland walichomoa moja kupitia kwa Robert Lewandowski, bao lililokuja kabla ya lile la pili la Gotze, lililomwacha kipa wa zamani wa Arsenal, Lukasz Fabianski anayekipiga pia Swansea, akishindwa kuzuia.

Jamhuri ya Ireland, katika kundi hilo hilo, waliwafunga Gibraltar 4-0 huku Scotland wakilala 1-0 kwa Georgia. Katika mechi ya mkondo wa kwanza, Ujerumani walilala kwa jirani zao wa Poland 2-0. Ujerumani, hata hivyo, wanaonekana kushuka kiwango uwanjani wakilinganishwa na walivyokuwa kwenye fainali za Kombe la Dunia.

Katika mechi nyingine, Ireland Kaskazini waliwafunga Visiwa vya Faroe 3-1, Finland wakawashinda Ugiriki 1-0, Hungary na Romania wakaenda suluhu sawa na ilivyokuwa kwa Denmark na Albania, huku Serbia wakiwaua Armenia kwa 2-0.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

STARS V NIGERIA: ADUI SI MUSA PEKE YAKE

Tanzania Sports

STARS YASHINDWA KUTAMBA NYUMBANI