Menu
in

Ngassa afanya majaribio na West Ham

Mshambuliaji wa pembeni wa Yanga na timu ya taifa, Taifa Stars, Mrisho Ngassa (Pichani), ameanza majaribio yake juzi kwenye klabu ya West Ham United ya Uingereza akiwa na hofu kutokana na kukutana na idadi kubwa ya wachezaji waliokwenda kufanya majaribio kwenye klabu hiyo.

Ngassa, ambaye alitua nchini Uingereza mwanzoni mwa wiki hii, alianza rasmi mazoezi akiwa na kikosi cha pili cha timu hiyo kilichochanganywa na wachezaji hao wanaojaribiwa, ambapo hali hiyo ilimfanya Ngassa kucheza kwa kutojiamini hali iliyosababisha wakala wake Yusuph Bakhresa kumtuliza presha.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo Nipashe imezipata kutoka kwa Bakhresa, imeelezwa kuwa siku ya kwanza ya majaribio yake Ngassa, hakuonyesha uwezo wake kutokana na kuwa na hofu hasa baada ya kuona idadi ya wanaofanyiwa majaribio ni kubwa.

Imeleezwa kuwa baada ya hali ile Bakhresa, alimtaka mchezaji huyo kucheza soka lake la kawaida na kuondoa hofu ushauri ambao aliutekeleza, ambapo jana alifanya mazoezi ya pamoja na kikosi cha kwanza cha West Ham.

Taarifa hiyo imeweka wazi kuwa baada ya ushauri huo Ngassa, alitulia na kucheza mpira wake wa kawaida, ambapo juzi alionyesha uwezo uliompa nafasi ya kujumuika na kikosi cha kwanza cha West Ham.

“Kidogo alipata wasiwasi katika siku ya kwanza ya majaribio yake, lakini aliwekwa sawa na sasa anaendelea vizuri na anaonyesha mchezo wake wa kawaida,”alisema Bakhresa.

Mchezaji huyo ataendelea kufanya majaribio na kikosi cha kwanza hadi pale atakapomaliza muda uliopangwa kwa ajili ya majaribio hayo.

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

Leave a Reply

Exit mobile version