in , , ,

Man U hoi, Chelsea kicheko

 

MSIMAMO wa Ligi Kuu ya England (EPL) katika nafasi tano za juu umebaki

bila kubadilika baada ya baadhi ya mechi za mzunguko wa 26.

Huku timu zilizo juu kabisa zikiwa bado na mechi 25, Jumamosi

imeshuhudia Manchester United wakifungwa 2-1 ugenini walikocheza dhidi

ya Sunderland.

Yalikuwa matokeo ya kusikitisha kwa kocha Louis van Gaal ambaye sasa

anasema kwamba huenda vijana wake wakaishia kucheza Ligi ya Europa

msimu ujao kutokana na kuzidiwa nguvu.

Sunderland waliongeza matumaini yao ya kujinusuru na kushuka daraja

baada ya Wahbi Khazri kutangulia kufunga bao dakika ya tat utu kwa

mpira wa adhabu ndogo ambao ulienda wavuni moja kwa moja.

Anthony Martial wa Man U alisawazisha akimzidi nguvu kipa wa zamani wa

Arsenal, Vito Mannone, aliyekuwa ameutema mpira wa Juan Mata.

Sunderland wanaofundishwa na Sam Allercyice ‘Big Sam’ hawakukubali

kuwaangusha watazamaji waliofika kuwaunga mkono, kwani Lamine

Konealifunga kwa kichwa kizuri mpira wa kona wa Khazri ambapo

ulimgonga kipa David de Gea na bao kuandikwa kwa jina la kipa huyo.

Huu ulikuwa ushindi wa kwanza katika EPL kwa Sunderland dhidi ya

Manchester United hapo kwenye Stadium of Light katika mechi 14.

United sasa wana pointi chache zaidi katika wakati kama huu kuliko

ilivyopata kuwa nazo kwenye EPL misimu iliyopita

Katika mechi nyingine, Chelsea wamevuna mabao matano dhidi ya

Newcastle na kuwatupa kwenye eneo la kushuka daraja, Chelsea walifunga

kupitia kwa Diego Costa, Pedro mawili, Willian na Bertrand Traore.

Newcastle walifuta machozi kupitia kwa Andros Townsend.

Katika mechi nyingine, Bournemouth wakiwa nyumbani walinyukwa na Stoke

3-1, Crystal Palace wakaangukia pua kwa 2-1 walipowakaribisha Watford.

Everton waliongea idadi ya timu zilizofungiwa nyumbani kwani walikula

1-0 kutoka kwa West Bromwich Albion sawa na Swansea kwa Southampton

wakati Norwich walilazimisha sare ya 2-2 mbele ya West Ham.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote
Tanzania Sports

SIMBA YAPAA KILELENI

Tanzania Sports

Arsenal waangusha mbuyu