Menu
in

Dan Mrwanda kuikosa mechi ya Taifa Stars.

Mshambuliaji peke wa timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) anaecheza soka la kulipwa nchini Kuwait Dan Mrwanda hatoweza kuja hapa kuichezea timu hiyo kwenye mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya timu ya taifa ya Congo DRC

Mchezo huo utachezwa jumamosi hapa jijini Dar es salaam kwenye dimba la Taifa na timu ya Congo DRC inawasili leo jumatano jioni.

Katibu mkuu wa Shirikisho la soka Tanzania (TFF) Fredrick Mwakalebela amesema wao waliandika barua kwa chama cha soka cha nchi hiyo kwenda kwenye timu anayochezea Mrwanda ili aweze kupata ruhusa ya kuja Tanzania kuichezea Taifa Stars ila hadi sasa bado hajapewa ruhusa hiyo

Pia Mwakalebela amesema pamoja na kukosa mchezo wa jumamosi dhidi ya DRC wao wanaendelea na mazungumzo ya kumtaka kuja hapa nchini kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya New Zeland utakaochezwa mwezi juni hapa nchini

Ili kuongeza muhimu wa mchezo huo TFF hivi sasa inataka pia kumshawishi yeye mwenyewe Mrwanda ili kuweza kuongeza changamoto kwa wakuu wa timu yake ili wamruhusu kuja kulitumikia Taifa lake

Mwisho kabisa Mwakalebela anasema wao wameandika barua kwa chama cha soka cha nchini Kuwait ili kuweza kumpata mshambuliaji huyo ila hadi sasa hawajapata majibu yeyote yale na wao bado wapo kimya hivyo hawajui nini kinaendelea

Kutokana na kumkosa Dan Mrwanda katika mchezo huo dhidi ya DRC kocha wa Taifa Stars Marcio Maximo atalazimika kuwatumia washambuliaji Jerry Tegete wa timu ya Yanga, Zahoro Pazi wa timu ya Mtibwa Sugar ya Morogoro pamoja na mshambuliaji mzoefu Mussa Hassan Mgosi wa timu ya Simba ya jijini Dar es salaam

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

Leave a Reply

Exit mobile version