in , ,

Costa Rica wawatungua Uruguay

 

Costa Rica wamewaadhiri Uruguay kwa kuwatungua mabao 3-1.

Katika mechi hiyo ambayo Uruguay walimpumzisha mshambuliaji machachari wa Liverpool, Luis Suarez, Uruguay walianza kupata bao kwa penati iliyopigwa na Edinson Cavani katika dakika ya 24.
Hata hivyo, mechi hiyo ya Kundi D walimo England na Italia ilibadilika kwa mshambuliaji wa Arsenal,
Joel Campbell kusawazisha katika dakika ya 54. Campbell anacheza kwa mkopo Olympiakos.

Dakika tatu baadaye, Costa Rica walipiga bao la pili kupitia kwa mlinzi wake, Oscar Duarte na kuwasisimua washabiki wao.
Kana kwamba hiyo haitoshi, akitokea benchi, Marcos Urena alinasa mpira wa Campbell na kumtungua kipa wa Uruguay, Fernando Muslera.

Mambo yalizidi kuwa mabaya kwa Uruguay kwa mchezaji wao, Maximiliano Pereira kupewa kadi nyekundu katika muda wa ziada kwa rafu isiyokuwa na lazima dhidi ya Campbell na sasa atakosa mechi ya Alhamisi dhidi ya England.

Report

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

What do you think?

71 Points
Upvote Downvote

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Loading…

0

Baloteli awaliza England

Malinzi asimamisha Uchaguzi Simba