Menu
in

BMT kukutana na TAHA

Baraza la michezo la taifa  hapa nchini Tanzania BMT kesho kutwa litakutana na  viongozi na wadau wa chama cha mchezo wa mpira wa mikono TAHA ili kupanga mikakati ya uchaguzi wa chama hicho.

Kaimu katibu mkuu wa baraza hilo, Mohamed Kiganja amesema mkutano huo utatoa tarehe ya kufanyika kwa uchaguzi huo ambao ulitakiwa kufanyika wiki iliyopita na kuhairishwa kutokana na kujitokeza kwa wagombea wachache katika kuwania nafasi za uchaguzi huo.

Aidha Kiganja amesema kumekuwepo na mwamko kwa wagombea na tayari jumla ya wagombea Kumi na sita

wamejitokeza kuwania nafasi mbalimbali katika chama hicho.

Hapo awali BMT ilisogeza mbele uchaguzi huo baada watu waliojitokeza kugombea nafasi kwenye chama hicho kutotimia huku baadhi ya nafasi zikikosa wagombea na sasa BMT inasema wagombea wamefikia idadi inayofa na ndio maana watajadili lini uchaguzi huo ufanyike.

Mikoa ambayo ni wanachama wa chama hicho ni mikoa miwili na vilabu ambapo wanachama wa chama hicho watakutana kuangalia suala la kuongeza idadi ya wanachama wa kupiga kura katika chama hicho.

Written by Israel Saria

For the last 20 years I have been working as a football pundit. This experience has provided me with a very useful insight into football and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics and I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany .....

Leave a Reply

Exit mobile version