Menu
in , ,

Rudisha ashinda mbio Uingereza

Mkenya David Rudisha amerejea katika makali yake kwa kutwaa ubingwa katika mbio za mita 800 za Diamond League jijini Glasgow, Scotland.
Hii ni mara ya kwanza kwa raia huyu wa Afrika Mashariki kupata ushindi katika ardhi ya Uingereza tangu alipopata medali ya dhahabu kwenye mbio za London 2012.

Rudisha (25) alikuwa nje kidogo kutokana na majeraha lakini sasa ameweka rekodi ya dunia kwa kuwatangulia wenzake kwa dakika nzima, akikimbia dakika 1:43.34.

“Najihisi mwenye furaha kubwa sana kwa sababu nipo vizuri sasa baada ya kuwa na mwaka mgumu lakini sasa nimejiweka sawa ndio maana nilikimbia kwa kasi kubwa,” anasema Rudisha ambaye atakuwa tena Hampden Park kwa ajili ya michuano ya Jumuiya ya Madola baadaye mwezi huu.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na Andre Olivier wa Afrika Kusini huku mshindi wa medali ya dhahabu wa Marekani, Allyson Felix na Mjamaica Shelly-Ann Fraser-Pryce walifuatia, nao wakiwa pia wanatoka kwenye majeraha.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version