Menu
in , , , ,

Liverpool waponea kwa Rovers

Liverpool wamefanikiwa kuingia nusu fainali ya Kombe la FA baada ya kuwafunga Blackburn Rovers 1-0.

Wakiwa wametoka kupigwa 4-1 na Arsenal kwenye Ligi Kuu wikiendi iliyopita na kufifia matumaini ya kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao, Liver walipata bao kupitia kwa Philippe Coutinho.

Mchezaji huyo wa Brazil alifunga pia kwenye mechi ya marudiano na Bolton katika raundi ya nne na sasa vijana hao wa Brendan Rodgers watachuana na Aston Villa katika Uwanja wa Wembley.

Hata hivyo, bado Liverpool hawakuonesha kiwango kikubwa kwenye mechi ya Jumatano hii, na yaweza kuonekana kwa nini walipoteza mechi zake dhidi ya Manchester United na Arsenal.

Nusu fainali ya kwanza ya FA ni baina ya Reading na Arsenal Aprili 18 na siku inayofuata ndipo Liver watacheza na Villa.

Kipa wa Liverpool, Simon Mignolet aliyeanza msimu chini ya kiwango aliokoa mabao mawili ya wazi kutoka kwa Tom Cairney na Ben Marshall.

Dakika za mwisho alimzuia kipa wa Rovers, Simon Eastwood aliyekaribia kufunga mpira wa kona.

Written by Israel Saria

I have been involved with sports in Tanzania as a Volleyball Coach for many years—and was a Tanzania Amateur Volleyball Association (TAVA) leader. I studied sports management at Leipzig University in Germany and understand the science behind sports. That led me to work as a football pundit, with the BBC ( Swahili service) in London. That experience and exposure took me to covering the 2010, World Cup in South Africa. This provided me with a great insight into international level football commentary and the opportunity to carry out extensive research into the game including its players, the stadiums, the rules and tactics.I have also been grateful to meet a wide range of people connected to football in the UK, Tanzania, Germany, Italy, Belgium, Ireland, France, Kenya etc, and visited almost all of the key football stadiums across United Kingdom, and Europe.

Leave a Reply

Exit mobile version